Chuo Cha Ualimu

Paradigms

Africa's Center for

Educational

Excellence!

 
`

KAULI YA MWENYEKITI WA BODI

“Nawahamasisha wazazi / walezi/watu binafsi wanaotaka kuwapatia vijana wao au kujipatia elimu bora kuchagua Chuo cha Ualimu Paradigms. Kwetu Paradigms elimu bora ni ile inayomuwezesha mwanafunzi kujijengea uwezo wa kiakili wa kuhoji masuala ya msingi kwa kujiamini kuwa anaweza, huku akithubutu kuchukua hatua mahsusi za kujiletea maendeleo.”

Prof. I. K. Bavu

 
 
 
 
Albamu ya Picha za Shule
Angalia picha za shule yetu. Bofya picha inayotiririka hapa chini uweze kupata picha zaidi.
 
 
 
Kuhusu Chuo Cha Ualimu PARADIGMS

image Paradigms


Inasomeka paradaimz
Ina maana ya mfano bora (a model / pattern)

 

 

Sisi ni akina nani?

Chuo cha ualimu Paradigms, ni chuo chenye kutoa elimu bora na kuaandaa walimu bora ambao ni mfano wa kuigwa.  Chuo kinatoa elimu na kuandaa walimu ngazi ya Stashahada, Cheti cha Daraja la 3 A na cheti cha Ualimu wa awali. Chuo kinapokea wanachuo wa kutwa na bweni, wavulana kwa wasichana.

 

 

Tuko wapi?


Chuo cha Ualimu Paradigms kipo kata ya Kimara, Mtaa wa Mavurunza, katika vilima vya Bonyokwa, Wilayani Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam. Chuo kimejengwa na kinaendelea kupanuliwa katika eneo la Ekari 25, linalomilikiwa, kupangwa na kuendelezwa na Paradigms Institute Ltd.

 

 

Tunafanya nini?


Tunafundisha masomo ya ualimu kulingana na mtaala wa Taasisi ya Elimu ya Taifa (Tanzania Institute of Education) unaotahiniwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA).